Friday, 28 August 2015
Monday, 24 August 2015
UWANJA WA NDEGE HATARI ZAIDI KUTUA DUNIANI!
Uwanja huo una barabara ya kurukia ndege na kutua (Runway 15/33) moja yenye urefu wa futi 6,445 (1,964 m) urefu ambao unalingana na viwanja vya mpira wa miguu 21 vyenye urefu wa mita 120 (393.6 ft),moja kati ya barabara za ndege kurukia na kutua fupi sana duniani. Una jengo moja la abiria lenye check-in counters 4,geti moja la kuingilia kwenye ndege na jengo la mizigo.
Sunday, 23 August 2015
Sakafu ya Bahari Siri Zake Zafunuliwa
TWAHITAJI kuelewa kindani kidogo
jinsi ambavyo dunia imeumbwa ili tuweze kuelewa mambo yaliyoonwa na
watafiti waliokuwa kwenye chombo cha Alvin. Yaaminika kuwa dunia yetu imefanyizwa na tabaka thabiti (linaloitwa lithosphere)
linalokalia mwamba ulioyeyuka, unaosogea polepole. Kwa wazi, tabaka
thabiti la nje lina kina cha takriban kilometa 100 nalo hufanyiza
asilimia 0.6 hivi tu ya dunia yote. Tabaka la nje kabisa, si laini, ni
nene mno chini ya mabara na jembamba kiasi cha kilometa sita chini ya
safu ya milima iliyo katikati ya bahari.
Ulimwengu Uliojaa Maajabu
MIAKA 100 hivi iliyopita, wanasayansi
waliamini kwamba ulimwengu mzima unapatikana katika kikundi chetu cha
nyota cha Kilimia. Hata hivyo, kwa sababu ya maendeleo makubwa ya
astronomia, fizikia, na tekinolojia katika karne ya 20 wanasayansi
wamegundua ukubwa halisi wa ulimwengu. Baadhi ya mambo ambayo wamegundua
yamewanyenyekeza. Kwa mfano, katika miaka ya hivi karibuni wataalamu wa
kuchunguza nyota wamegundua kwamba hawajui kile kinachofanyiza zaidi ya
asilimia 90 ya ulimwengu. Isitoshe, ugunduzi ambao umewafanya wafikie
mkataa huo umewaacha wanasayansi wakijiuliza ikiwa kweli wanaelewa
kanuni za msingi za fizikia. Maswali kama hayo si mageni.
Friday, 21 August 2015
Viumbe Hatari Kabisa Duniani, Anayeshika Namba Moja Ni Mbu!
Simba,
Nyati, Faru, Chatu....haya ndiyo majina ya wanyama yanayoweza kukujia
akilini pindi ukiulizwa MNYAMA YUPI NI HATARI ZAIDI KWA MWANADAMU. Well,
amini usiamini, kiumbe hatari zaidi ni mdogo mara elfu kadhaa
akilinganishwa kiumbo na hao majabali tunaowafahamu. Na udogo wake si
katika umbile pekee bali pia hata sauti yake ni ndogo kulinganisha na
mbwa, paka au mbuzi, achilia mbali wababe kama Simba, Chui au Faru.
Kiumbe huyo hatari wa kuogopwa kwa gharama yoyote ile ni MBU.
Viumbe wa ajabu wa baharini
WATU wengi wanadhani kuwa utafiti kuhusiana na wanyama umekamilika.
Lakini ukweli ni kuwa bado kuna maswali mengi sana kuhusiana na maisha
ya wanyama mbalimbali ambayo hayajapatiwa majibu.
Ndio maana kila kukicha unajitokeza ugunduzi mwingine mpya ambao mara
nyingi unawaacha watafiti vinywa wazi lakini baadaye unatoa mwanga wa
masuala kadhaa waliyokuwa hawayaelewi awali.
Mathalani, tunafahamu visa kadhaa vya watoto kuzaliwa wakiwa wameungana.
Lakini hivi karibuni watafiti wa huko Mexico walimgundua nyangumi wa
kijivu walioungana.
Monday, 20 July 2015
Wednesday, 8 July 2015
Saturday, 4 July 2015
Subscribe to:
Posts (Atom)





