Pages

Friday 22 August 2014

RIHANNA KUINUNUA LIVERPOOL


Mapenzi ya Rihanna kwenye soka yameingia katika hatua nyingine na sasa hataki kuwa shabiki tu bali mmiliki halali wa timu kubwa duniani, na kwa kuanza anataka kuinunua Liverpool FC!
Kwa mujibu wa gazeti la Hispania, El Mundo Deportivo mwimbaji huyo alianza mpango huo muda mfupi baada ya kuisha kwa fainali za kombe la dunia nchini Brazil ambapo alionekana akitweet mara kwa mara kuhusu mechi zilizokuwa zinaendeelea.


Gazeti hilo limeeleza kuwa Rihanna amekuwa akipata ushauri kutoka kwa marafiki zake wa karibu akiwemo mchezaji wa Chelsea, Didier Drogba ili kufanya maamuzi sahihi katika ununuzi wa club ya mpira wa miguu.
Kwa sasa Liverpool inamilikiwa na John W. Henry na hana mpango wa kuiuza timu hiyo ya soka. 

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets