Pages

Friday 28 November 2014

FUATILIA MAJIBU YA SERIKALI HAPA;Majibu ya serikali kuhusu ripoti ya PAC (click)

Habari wakuu,
Baada ya jana ripoti kusomwa, Kama kawaida moja kwa moja kutoka bungeni Dodoma tutajuzana hapa kupitia habari clan. Kwa wale wasio na uwezo kufatilia moja kwa moja pia kwa wale wenye nafasi ya kufatilia lakini wakapenda kuona mirejesho fursa ambayo haipo kwenye vyombo vingine vya habari. Tuungane kwa pamoja katika ngwe ya leo kutoka Dodoma.

Wednesday 26 November 2014

Maneno ya Wabunge Novemba 20 2014 bungeni kuhusiana na mamlaka za bunge na mahakama.

PoliticsKama haukusikiliza ama kutazama Kikao cha Bunge Dodoma leo, moja ya masuala yaliyotawala ni kuhusu Mamlaka ya Bunge na Mahakama, wa kwanza kuzungumza alikuwa David Kafulila; “… Naomba mwongozo kuhusiana na taarifa ya PAC kuhusiana na sakata la ufisadi wa ESCROW kama italetwa ama haitaletwa na msingi wa swali lile ulikuwa ukizingatia kwamba zimekuwepo taarifa za mkakati wa kuhakikisha Mahakama inatumika kuhakikisha ripoti ile hailetwi Bungeni na kufikia mwisho…”

Mapokezi ya Mbunge David Kafulila Bungeni leo Novemba 24 baada ya kufunga Ndoa


Kafulila-ndoa-pic2Siku ya Jumamosi Novemba 22 millardayo.com ilikupatia taarifa kuhusu Mbunge David Kafulila kufunga Ndoa Kigoma, leo Novemba 24 kaingia ndani ya Jengo la Bunge Dodoma na kupigiwa shangwe za mapokezi na Wabunge wa Bunge hilo wakati kikao kikiwa kinaendelea.
Spika wa Bunge Anne Makinda alikuwa kwa kwanza kuzungumza wakati Wabunge wakimpigia makofi David Kafulila alipokuwa anaingia; “… Bwana Harusi anaingia… Sasa Bibi Harusi yuko wapi mimi nilitegemea anakuwa pale… Mchezo mbaya huo.. Haya asante nashukuru, hongera…“- Anne Makinda.
Naibu Waziri wa Mawasiliano Sayansi na Teknolojia January Makamba naye aliongea haya; “… Na mimi napenda kuchukua fursa ya kumpongeza Mheshimiwa David Kafulila kwa kuoa, karibu kwenye klabu yetu na hongera sana…'
like page yetu hapa

Thursday 20 November 2014

SWAGA ZILIKUWA ZAMANI BWANA, KUNA SWAGA SIKU HIZI?

Mandeleo yameua swaga nakwambia. Watu siku hizi wanajidaiii eti wana swaaga, aa wapi!! swaga zilikuwa zamani bwana. Enzi hizo za redio moja, mtu ukitoka kijijini na kuweza kuja kukaa mjini hata wiki moja tu, ukirudi unajikuta wewe ndie mjanja wa kijijini, na kama ulibahatika kuja jiji la Dar es Salaam, basi

NALAANI MAPEPO YOTE YA ATM

1798805_womanatm_jpeg09f78e300bf098e76a7e50d5bad65e2bNalaani mapepo yote yanayofanya nishindwe kutoa pesa, nafunga minyororo mapepo yaliyofanya nisahau password, shindwa shindwa shindwa kabisa….emeeeeeeen
LIKE PAGE YETU HAPA

TATIZO LILITOKEA MIAKA KUMI ILIYOPITA

 
Jamaa alivunjika mguu akaepelekwa hospitali;
DAKTARI: Imekuwaje mpaka ukavunjika mguu?
JAMAA: Miaka kumi iliyopita…
DAKTARI: Staki kujua hayo nataka kujua umevunjikaje mguu?
JAMAA: Dokta nisikilize kwanza, miaka kumi iliyopita nilikuwa nafanya kazi kwa bosi moja kule Uzunguni, siku moja binti yake mzuri sana akaja chumbani kwangu na kuniuliza kama nahitaji kitu chochote, nikamjibu sitaki, akarudia tena tena na kuniuliza tena kama sihitaji kitu chochote, mimi nikasema sihitaji kitu, akaondoka anacheka.
DAKTARI: Sasa hiyo inauhusiano gani na kuvunjika mguu?
 JAMAA:Sasa leo nilipokuwa niko juu ya mnazi nagema, si ndio jibu likanijia kwanini yule mrembo alikuwa ananiuliza lile swali, ndio bahati mbaya nikajisahau nikaanguka na kuvunjika mguu 
like page yetu kwa vichekesho zaidi
 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets