Pages

Thursday 30 April 2015

Sayari 10 Zinazoweza kuwa na Maisha

Mpaka kufikia Aprili 2014, kuna Sayari 21 nje ya mfumo wetu wa Jua, ambazo zina uwezekano mkubwa wa kuwa na maisha ukiachana na Sayari yetu (Dunia).
Katika sayari hizi 21, zipo ambazo wanaSayansi hawana uhakika zaidi, kwani wanaendelea kuzisoma mazingira yake.
Ifuatayo ni orodha ya Sayari 10, ambazo mpaka sasa; zina uwezekano mkubwa zaidi wa kuwa na namna fulani ya maisha/ viumbe hai.
image

Monday 20 April 2015

MPOGORO MGANGA NA MCHAGA

Image result for mganga
Mpogoro alitangaza anatibu magonjwa yooooooote kwa tsh. 100000/=
Na kama akishindwa kukutibu angekurudishia laki yako nakukuongeza laki nyingine.

Tazama chanzo cha Nyota


'''Nyota''' kwa lugha ya kawaida ni nuru ndogo zinazoonekana angani wakati wa usiku.

== Nyota ni magimba makubwa ==
Kwa kutumia darubini na vifaa vya kisasayansi imegunduliwa ya kwamba ni magimba makubwa sana katika [[anga la nje]] yanayong'aa kwa sababu yanatoa mwanga, joto na aina mbalimbali za [[mnururisho]] kutokana na [[myeyungano ya kinyukilia]] ndani yao. Lakini ziko mbali sana na kwa hiyo tunaziona kama nukta ndogo za nuru. Kwa jumla nyota zinaonekana kwenye anga kwa mpangilio usiobadilika na kila nyota huwa na mahali pake pasipobadilika kati ya nyota nyingine hata kama nyota kwa jumla zinazunguka angani juu yetu kila siku.

Saturday 18 April 2015


Jua ni nyota iliyopo karibu zaidi  na sayari yetu ya Dunia kuliko nyota nyingine zote. Kuwa karibu na Dunia kumesababisha nuru au miale yake kuleta joto na mwanga katika uso wa dunia  kuliko nyota nyingine tunazoziona.

Hali ya Pekee ya Jua Letu


UNAPOSOMA makala hii, huenda jua limechomoza au huenda unajua litachomoza baada ya muda mfupi. Je, hilo ni jambo muhimu? Naam, kwa sababu pasipo nuru ya jua, matrilioni ya viumbe walio duniani—kutia na wewe—hawangekuwapo.  Mamilioni ya viumbe mbalimbali, kuanzia kwa bakteria wenye chembe moja hadi nyangumi wakubwa mno wangeangamia wote.

Mabadiliko katika Mwonekano wa Zuhura Angani Mabadiliko katika Mwonekano wa Zuhura Angani




Ukweli Kuhusu Mbingu

WATU fulani wanafikiri kwamba hatuwezi kujua ukweli kuhusu mbingu kwa sababu hakuna mtu ambaye ameshuka kutoka huko ili atueleze mambo ya mbinguni. Labda wamesahau kwamba Yesu alisema hivi: “Nimeshuka kutoka mbinguni.” (Yohana 6:38) Pia, aliwaambia hivi viongozi fulani wa kidini: “Ninyi mnatoka kwenye makao ya chini; mimi ninatoka kwenye makao ya juu.” (Yohana 8:23) Yesu alisema nini kuhusu mbingu?

Friday 10 April 2015

UNAMFAHAMU MNYAMA MZITO KULIKO WOTE DUNIANI?uzito wa ulimi wake ni sawa na uzito wa TEMBO mmoja


NYANGUMI WA BLUU AU the  blue whale ni mnyama aishie baharini na ana urefu wa mita 30 na uzito wa kilo hadi 201,000 au tani 210 na zaidi,ni mnyama mkubwa na mzito kuliko yeyote aliyewahi kutokea duniani.

Je wajua wanyama wakubwa baarini?

Wanyama Wakubwa wa Baharini
 
Mnyama mkubwa anaibuka kutoka baharini, ananyakua mashua nzima, na kuivuta pamoja na mabaharia chini ya maji. Hadithi kama hizo zimesimuliwa kwa miaka mingi sana. Lakini je, wanyama hao wakubwa ni halisi?
MNAMO 2007 ngisi anayeitwa colossal alishikwa bila kukusudia na wavuvi katika Bahari ya Ross karibu na Antaktika. Alikuwa na urefu wa mita 10 hivi, kutia na minyiri yake, na alikuwa na uzito wa karibu kilogramu 500! Wanasayansi wanaamini kwamba aina hiyo ya ngisi wanaweza kuwa wakubwa hata zaidi.
Mnyama mwingine mkubwa kama huyo anaitwa ngisi-jitu ambaye ana mwili wenye umbo la kombora, macho yenye ukubwa wa kichwa cha mwanadamu, mdomo kama wa kasuku wenye nguvu za kukata nyaya za chuma, mikono minane yenye mashimo ya kufyonza, na minyiri miwili mirefu ya kuvuta chakula hadi mdomoni. Akiwa majini anaweza kusonga kwa mwendo wa kilomita 30 kwa saa, na hata anaweza kujirusha hewani!
Katika karne iliyopita inasemekana kwamba wanyama hao wakubwa walionekana mara zisizozidi 50, na hawajawahi kufanyiwa uchunguzi wakiwa baharini.

Wanasayansi wagundua bahari Sayari ya Mars


    NI HATUA NZURI YA UWEZEKANO WA BINADAMU KWENDA KUISHI, DALILI ZAONYESHA KUNA VIUMBE HAI
    Image result for bahari katika mars
    WANASAYANSI wa anga kwa muda mrefu wamekuwa wakitafuta uwezekano wa maisha katika sayari nyingine, mbali na dunia.Kuna imani kuwa kwenye sayari hizo, huenda zikapatikana raslimali nyingi kwa urahisi kuliko duniani ambako binadamu wameishi mamilioni ya miaka hadi sasa.
    Wataalamu hao wa anga wamekuwa wakifanya hivyo kwa muda sasa na moja ya mambo muhimu wanayoangalia ni upatikanaji wa maji. Popote maji yanapopatikana, wanaamini maisha yanawezekana.Moja ya sayari ambayo wamekuwa wakiichunguza kwa miaka mingi sasa ni Mars, ambayo ni ya nne kutoka kwenye jua. Dunia ni ya tatu.
    Sababu kuu za kuichagua sayari hii tofauti na zingine ni kwamba, hali ya hewa inatofautiana kidogo sana na ya dunia.

Wednesday 8 April 2015

Je wajua vituko vya whatsap wiki hii? hangalia hapa


RAIS JK AANIKA MAGUMU KATIKA UTAWALA WAKE!




Dar es Salaam. Wakati makada wa CCM wakipigana vikumbo kuwania kupitishwa na chama chao kuwania urais, Rais Jakaya Kikwete anayemaliza ngwe yake amesema nafasi hiyo ni kadhia, ni kazi ngumu na si ya kukimbilia.

Rais Kikwete aliyasema hayo juzi nchini Marekani, wakati akihutubia kwenye taasisi inayoitwa, Woodrow Wilson International Center for Scholars, ambapo alitumia muda huo kuelezea mafanikio na changamoto katika kipindi chake cha miaka 10 ya uongozi wake.

Friday 3 April 2015

Vyombo vinavyoongozwa kwa fahamu zetu tu

Katika miaka ya hivi karibuni, tumeona teknolojia ikikua kwa kasi ya ajabu mno.
Mambo ambayo hapo nyuma yalionekana kama ndoto au stori tu, sasa yameweza kufanywa kuwa Halisia.Na bado teknolojia hii yaendelea kukua kila iitwapo leo.
Leo ningependa kuongelea teknolojia ambayo inamuwezesha mtu kukiongoza (ku-control) kifaa fulani kwa kufikiri/kwa mawazo tu.
Ni kitu ambacho wengi hukiona kwenye movie tu (haswa kwa wale wenzangu na mimi ambao hupenda movie na tamthilia za Sci-Fi). 
image

Kwanini Pluto si Sayari?

Kama wewe ni miongoni mwa watu wa rika moja na mimi… Utakumbuka kuwa: Katika somo la Sayansi tulijifunza kuwa Pluto ni sayari ya mwisho katika mfumo wetu wa Jua. Lakini baada ya muda si mrefu ukakoseshwa mtihani kwa kujibu Pluto ni Sayari.
Pengine uliambiwa kwanini Pluto si sayari tena, au pengine mpaka leo ulikuwa unadhani Pluto ni moja ya sayari katika Mfumo wetu wa Jua…
Karibu tuiangalie kwa Undani Historia

Je Wajua?

Mwezi mkubwa kuliko miezi yote katika mfumo wetu wa Jua ni ‘Ganymede’. Mwezi huo ni mkubwa kuliko hata sayari ya Utaridi (Mercury)
image

Je wajua Sayari 10 Zinazoweza kuwa na Maisha?

Mpaka kufikia Aprili 2014, kuna Sayari 21 nje ya mfumo wetu wa Jua, ambazo zina uwezekano mkubwa wa kuwa na maisha ukiachana na Sayari yetu (Dunia).
Katika sayari hizi 21, zipo ambazo wanaSayansi hawana uhakika zaidi, kwani wanaendelea kuzisoma mazingira yake.
Ifuatayo ni orodha ya Sayari 10, ambazo mpaka sasa; zina uwezekano mkubwa zaidi wa kuwa na namna fulani ya maisha/ viumbe hai.

WATU WAWILI WANASHIKIRIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUFUKUA KABURI LA ALBINO NA KUMNYOFOA VIUNGO WILAYANI KARAGWE MKOANI KAGERA

JESHI la Polisi mkoani Kagera, linawashikilia watu wawili wakituhumiwa kufukua kaburi la marehemu Baltazar  John mwenye ulemavu wa ngozi (albino) na kuchukua viungo viungo vyake.
 Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Henry Mwaibambe, tukio hilo limetokea 27 Machi mwaka huu, ambapo watuhumiwa walinaswa katika nyumba ya kulala wageni ya Ford iliyopo eneo la Kyaka wilayani Missenyi.

Wataalamu wasema joto la dunia laongeza frikwenzi za radi na ukali

WATAFITI  wa masuala ya anga wamesema kwamba ongezeko la joto duniani linachangia ongezeko la  milipuko  ya radi katika maeneo mbalimbali duniani.
Katika taarifa yao ya utafiti huo iliyochapishwa katika jarida la sayansi wamesema ongezeko hilo limechangia kuongezeka kwa radi.
Utafiti huo uliofanywa kwa kuangalia takwimu kutoka katika mtandao wa vizuia radi,timu ya wataalamu wameangalia kwa udani ongezeko la joto na ongezeko la milipuko ya radi.
"Katika milipuko miwili ya radi katika 2000, kutakuwa na milipuko mitatu kwenye 2100," anasema David Romps, wa Chuo Kikuu cha California, Berkeley.
Pamoja na milipuko hiyo kuanzisha mioto katika mbuga zilizokavu, milipuko hiyo hubadili kemia ya anga.
Kundi hilo la wataalamu pia limebainisha njia mpya ya kuangalia uhusiano kati ya joto na milipuko ya radi, kuw akukadiria joto lililopo linalowezesha kuwepo kwa mawingu ya radi.
"Huku joto la dunia likiongezeka vichocheo hivi vya radi navyo vinaongezeka na radi inapotengenezwa  mlipuko wake utakuwa na nguvu zaidi,"  anasema profesa Romps.
Yeye na wataalamuw enzake wamepiga hesabu kwamba kwa kila ongezeko la joto katika dunia 1C  kutasababisha kuwepo na ongezeko la mkilipuko kwa asilimia 12.
Walithaminisha takwimu zao kwa kuangalia kwa kipindi cha mwaka mzima takwimu zilizokusanywa na  Mtandao wa Vipinga Radi nchini Marekani (US National Lightning Detector Network) ambavyo hunasa kila mrusho wa sumaku elektroniki, unaosababishwa na milipuko ya radi nchini Marekani.
Alisema matokeo ya takwimu hizo ni ya kusisimua sana kwani muda, mahali ya milipuko hiyo imerekodiwa kisahihi kabisa na kutoa takwimu zilizo sahihi zinazoonesha mfadhaiko wa dunia katika siku zijazo.
Ingawa nusu ya mioto katika mapori ya Marekani husababishwa na milipuko ya radi, kila mlipuko una nguvu ya kutosha kutengeneza mzunguko wa kikemikali na  nitrogen oxides.
Radi inatengenezwa vipi

Wataalamu wagundua sayari inayofanana na yetu, hatuwezi kufika

MOJA kati ya sayari nane mpya zilizo nje ya mfumo wa jua (letu) imeonekana kuwa na mazingira kama dunia yetu.
Sayari hizo ambazo ziko umbali wa miaka ya mianga 475 zimeonwa na darubini maalumu ya kuangalia mifumo ya nyota mbali na nyota yetu, inayomilikiwa na Wamarekani ya Kepler.
Kwa Mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Anga za Juu la Marekani (NASA)  imesema sayari tatu zinafanana na dunia yetu kutokana na hesabu za umbali kutoka katika jua (lao) lakini moja ndio inaonekana kuwa na  mazingira yanayofanana na dunia na ina joto la juu kidogo.
Taarifa hiyo ya wataalamu wanaoangalia taarifa kuhusu sayari nyingine nje ya mfumo wa sayari yetu zimetolewa katika mkutano wa wanajimu wa Marekani(American Astronomical Society)
Sayari hizo 3 ambazo zimeingia katika jedwali la Kepler zinafanya sayari zinazoonekana kufaa kama dunia yetu kuwa nane.

Thursday 2 April 2015

PASAKA NI NINI NA MAANA YAKE


Pasaka ni sikuku iliyoamriwa na Mungu tangu siku za kale kwa wayahudi kuifanya katika mwezi wa Abibu au Nisani katika “kalenda ya kiebrania” yaani mwezi wa 3 au 4 katika kalenda ya kirumi, kwa lengo la kumbuka njisi Mungu alivyowakomboa kutoka utumwani Misri; Twasoma: “Utunze mwezi wa Abibu, ukamfanyie pasaka BWANA, Mungu wako, kwa kuwa ilikuwa ni mwezi wa Abibu alipokutoa Misri usiku BWANA; Mungu wako. Nawe umchinjie pasaka BWANA, Mungu wako katika kundi la kondoo na la ng’ombe, mahali atakapochagua BWANA apakalishe jina lake.” (Kumbukumbu 16:1-2) Soma pia: (Kutoka 12:14) Kama tulivyoona katika pasaka wayahudi waliamriwa kuchinja mnyama mmoja katika kundi, lakini tunapoendela kusoma tunaona jinsia Mungu alivyoamuru mnyama huyo aokwe na kuliwa; Twasoma:
“Usimle pamoja na mikate iliyotiwa chachu; siku saba utakula naye mikate isiyotiwa chachu, nayo ni mikate ya mateso; kwa maana ulitoka nchi ya Misri kwa haraka; ili upate kukumbuka siku uliyotoa nchi ya Misri, siku zote za maisha yako. Wala isionekane kwako chachu muda wa siku saba katika mipaka yako yote; wala katika hiyo nyama uchinjayo siku ya kwanza jioni, kisilale cho chote usiku kucha hata asubuhi. Usimchinje pasaka ndani ya malango yako yote akupayo BWANA, Mungu wako; ila
mahali atakapochagua BWANA, Mungu wako apakalishe jina lake, ndipo mtakapomchinjia pasaka jioni, katika machweo ya jua, kwa wakati kama uliotoka Misri.” (Kumbukumbu 16:3-6); Soma pia: (Kut 12:3-13) Katika mwezi huo wa abibu ambao Mungu aliufanya kuwa mwezi wa kwanza kwako, Wayahudi walifanya karamu ya Pasaka kuwa kumbukumbu la jinsi Mungu alivyowaokoa kutoka Misri (Kutoka 12:1-51; Walawi. 23:5).

Ukweli wa Kustaajabisha Kuhusu Nyota za Angani

Watu wanapofikiri kuhusu ulimwengu basi wanafikiria nyota. Nyota ndizo zinazofanya sehemu kubwa ya yabisi, kiminika na hewa (matter) inayoonekana na ingawa nyota zote mbali na jua ziko katika umbali usiofikirika kutoka tulipo, bado tunaweza kuziona nyotamaelfu kwa maelfu kwa macho yetu wenyewe. Kuna maajabu mengi ya ukweli kuhusu nyota lakini nitaongelea machache yanayovutia na wengine wanaweza kuongezea ili tijifunze au kueleweshana pamoja.
1.Idadi ya nyota katika ulimwengu unaoonekana

Katika usiku wenye giza tororo katika maeneo ya vijijini au mbali na mji unaweza kujionea nyota zisizo na idadi lakini katika mazingira ya kawaida hapo unakuwa unaangalia nyota kama 2500 na si zaidi ya hapo. Hizo ni moja ya billioni 1/100,000,000 ya jumla ya nyota zilizo katika galaxi tuishiyo (MilkyWay).
Milky way ni moja ya galaxi kubwa sana katika universe na sisi tumebahatika kuwa ndani ya galaxi hii. Labda kidogo tuangalie kwa kifupi ukweliwa galaxi hii. Diameter (kipenyo) ya Milky Way kutoka upande mmoja mpaka mwingine ni umbali wa miaka laki moja (100,000) ya mwendo wa mwanga. Mwendo wa mwanga kwa mwaka ni jinsi mwanga unavyosafifi kwa mwaka mzima kutoka point moja mpaka nyingine. Mwanga husafiri kwa mwendo wa kasi kuliko mwendo wa kitu kingine chochote tunachokijua. Kwa mfano katika sekunde moja mwanga unasafiri umbali wa kuzunguka dunia mara saba. Hivyo mwaka mmoja wa kusafiri kwa mwanga (a light year) ni umbali wa kustaajabisha. Inaweza kuchukua miaka elfu kumi na nane kwa chombo chenye kasi zaidi cha anga kusafiri mwaka mmoja wa mwanga. Sasa hapa ku-cover distance ya kipenyo cha MilkyWay tunazungumzia umbali wa miaka 100,000 ya kusafiri kwa mwanga.
Hii pia ina maana unapochukua telescope ukafanikiwa kuziona nyota zilizoko upande mwengine wa mwisho wa galaxi, basi unaziona jinsi zilivyokuwa miaka 100,000 iliyopita, kwa sababu mwanga uliotoka kwenye nyota hizo miaka laki moja iliyopita ndio kwanza unatufikia. hii ni sawa pia kwamba kama kuna kiumbe katika upande mwingine wa galaxi na anaiangalia dunia kwa telescope basi ataiona dunia kama ilivyokuwa miaka 100,000 iliyopita.
 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets