Pages

Friday 3 April 2015

WATU WAWILI WANASHIKIRIWA NA JESHI LA POLISI KWA KUFUKUA KABURI LA ALBINO NA KUMNYOFOA VIUNGO WILAYANI KARAGWE MKOANI KAGERA

JESHI la Polisi mkoani Kagera, linawashikilia watu wawili wakituhumiwa kufukua kaburi la marehemu Baltazar  John mwenye ulemavu wa ngozi (albino) na kuchukua viungo viungo vyake.
 Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Kagera, Henry Mwaibambe, tukio hilo limetokea 27 Machi mwaka huu, ambapo watuhumiwa walinaswa katika nyumba ya kulala wageni ya Ford iliyopo eneo la Kyaka wilayani Missenyi.

Watuhumiwa hao ni Laston Faustine (41) mkazi wa Lukulaijo na January Korongo (43) wakazi wa Kadengesho wilayani Karagwe mkoani Kagera, ambapo walikutwa na mifupa mitatu ya binadamu.
Kamanda Mwaibambe amesema “katika mahojiano mtuhumiwa wa kwanza- Faustine, alituambia kuwa alipewa viungo hivyo na Korongo kwa ajili ya kuviuza Sh. 20 milioni.”


Ameongeza kuwa, Korongo alipohojiwa amekiri kwamba alifukua kaburi la mjomba wake aitwae Baltazari John (albino), ambaye alifariki mwaka 1991 na mwili wake kufukuliwa 2009.

“Baada ya kumuhoji zaidi mtuhumiwa huyo, alikubali kuongozana na polisi hadi nyumbani kwake ambapo alionyesha fuvu la kichwa, mifupa mitatu ya miguu pamoja na mifupa ya sehemu mbalimbali ambayo ilikuwa imefungwa kwenye mfuko nje ya nyumba yake.


“Ili kujiridhisha, jeshi liliomba kibali cha mahakama wilayani Karagwe ili kufukua kaburi hilo kuhakikisha kama kweli kuna mabaki ya mwili huo. Tulipofukua hakuna kilichopatikana,” amesema kamanda.

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets