Pages

Friday 3 April 2015

Wataalamu wasema joto la dunia laongeza frikwenzi za radi na ukali

WATAFITI  wa masuala ya anga wamesema kwamba ongezeko la joto duniani linachangia ongezeko la  milipuko  ya radi katika maeneo mbalimbali duniani.
Katika taarifa yao ya utafiti huo iliyochapishwa katika jarida la sayansi wamesema ongezeko hilo limechangia kuongezeka kwa radi.
Utafiti huo uliofanywa kwa kuangalia takwimu kutoka katika mtandao wa vizuia radi,timu ya wataalamu wameangalia kwa udani ongezeko la joto na ongezeko la milipuko ya radi.
"Katika milipuko miwili ya radi katika 2000, kutakuwa na milipuko mitatu kwenye 2100," anasema David Romps, wa Chuo Kikuu cha California, Berkeley.
Pamoja na milipuko hiyo kuanzisha mioto katika mbuga zilizokavu, milipuko hiyo hubadili kemia ya anga.
Kundi hilo la wataalamu pia limebainisha njia mpya ya kuangalia uhusiano kati ya joto na milipuko ya radi, kuw akukadiria joto lililopo linalowezesha kuwepo kwa mawingu ya radi.
"Huku joto la dunia likiongezeka vichocheo hivi vya radi navyo vinaongezeka na radi inapotengenezwa  mlipuko wake utakuwa na nguvu zaidi,"  anasema profesa Romps.
Yeye na wataalamuw enzake wamepiga hesabu kwamba kwa kila ongezeko la joto katika dunia 1C  kutasababisha kuwepo na ongezeko la mkilipuko kwa asilimia 12.
Walithaminisha takwimu zao kwa kuangalia kwa kipindi cha mwaka mzima takwimu zilizokusanywa na  Mtandao wa Vipinga Radi nchini Marekani (US National Lightning Detector Network) ambavyo hunasa kila mrusho wa sumaku elektroniki, unaosababishwa na milipuko ya radi nchini Marekani.
Alisema matokeo ya takwimu hizo ni ya kusisimua sana kwani muda, mahali ya milipuko hiyo imerekodiwa kisahihi kabisa na kutoa takwimu zilizo sahihi zinazoonesha mfadhaiko wa dunia katika siku zijazo.
Ingawa nusu ya mioto katika mapori ya Marekani husababishwa na milipuko ya radi, kila mlipuko una nguvu ya kutosha kutengeneza mzunguko wa kikemikali na  nitrogen oxides.
Radi inatengenezwa vipi
Bado haijajulikana nini hasa inasababisha radi, lakini wanasayansi wanaamini kwamba ili kuwepo na radi ni lazima katika mada zake zote yaani  mvuke,kimiminika na barafu ni lazima yawepo.
Mawingu ni lazima yaumuke kwa haraka kuwezesha kunyanyua kimiminika na barafu na  kuvining’iniza.
Wakati mabonge madogo ya barafu yanagongana yuanasababisha uwapo wa electron ambazo zinasababisha kuwepo kwa nishati, ambapo mabonge ya garafu yenye nishati hasi yakienda chini na zile chanya zikienda katika mabonge madogo zaidi yaliyopo juu. Mwishoni wataalamu wanasema kwamba ni lazima kuwepo na kutenganishwa kwa pande hizo mbili ambapo nishati hasi inaporomoka kwa nguvu na kusababisha mwale wa radi.
Profesa Romps anasema kwamba chanzo kikuu cha gesi ya nitrogen oxide katika troposphere ya kati na ya juu ni radi
Kuwepo kwa gesi hii kwa namna Fulani inadhibiti gesi zinazotengeneza anga linalohami dunia ikiwamo ozone na methane.
Prof Romps anasema  hali hiyo ni tukio kubwa kwa kile kitu kinachoitwa kupanda kidogo kwa joto, lakini akasem,a kama joto la dunia litapanda kwa 4c katuika karne ya 21 mabadiliko katika uwingi wa milipuko ya radi itakuwa ndio msingi wa mashaka ya binadamu kwani itaenda kujaza hewa zisizotakiwa.
Alisema kiasi kikubwa cha hewa ya kaboni kinachotupwa katika anga katika karne hii kitakaa  pale kwa miaka 100,000

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets