Kikundi cha wanajiolojia watafiti

Katika makala haya, tutaangalia jinsi wanasayansi wa kawaida, tena ambao walikuwa hawaamini  kabisa kwamba kuna Mungu au shetani, katika utafiti wao ambao haukuwa na uhusiano wowote na masuala ya rohoni, walijikuta wanagundua mambo ambayo yaliwatia hofu hadi wengine kukimbia kazi. Waliweza kusikia waziwazi sauti za vilio vya mateso kutokea katikati ya dunia! Sauti hizo walizirekodi; na mwisho wa makala haya utaona anwani inayoweza kukupeleka kuzisikia sauti hizo za kutisha na kusikitisha mno, mno!!

Ni nani ambaye hajasikia habari za kwamba wanga huenda baharini, wakatupa mayai viza kisha malango yanafunguka nao wanashuka hadi kuzimu? Bila shaka habari hizi si ngeni masikioni mwa wengi wetu? Ni mambo ambayo ni rahisi kuaminika katika ulimwengu wa kawaida lakini unapoyaongelea kwa mtazamo wa Biblia, hapo watu wanaanza kukosa imani na kudhani kuwa si za kweli.

Makala haya yanatokana na habari ambayo iliandikwa katika gazeti la Ammennusatia la kule Finland katika toleo lake la Julai 1989.

       Sehemu ya gazeti

Kikundi kimoja cha wanajiologia (wana elimu ya miamba) wa Kirusi walikuwa katika mradi wa kutoboa tundu katika eneo la Kola, karibu na Murmansk; maili takriban 150 kaskazini mwa Duara la Aktiki, nchini Siberia. Watafiti hao waliweza kutoboa tundu ardhini lenye urefu wa kilometa 14.4 kwenda chini.

Dr Azzacov, ambaye alikuwa ndiye meneja wa mradi alisema kuwa wakati wa kutoboa, ghafla drili ilianza kuzunguka bila utaratibu, hali iliyoonyesha kwamba drili imefika kwenye sehemu iliyo na uwazi.