Pages

Tuesday 30 December 2014

Jamaa mmoja alienda kuposa kwa mzee mmoja

Mzee: Yaani wewe umekuja kuposa huku unatafuna big G? Si dharau hiyo!  
Jamaa: Natoa harufu ya sigara.  
Mzee: Unasemaje? Unavuta sigara pia!?  
Jamaa: Nikitoka klabu kulewa ndo huwa navuta. Mzee: Tobaa! Unalewa!?  
Jamaa: Nilianza kulewa nilipokuwa jela.  
Mzee: Yaani na kufungwa pia umeshawahi!?  
Jamaa: Ah si niliua mtu.
Mzee: Duh kumbe wewe muuaji!? Astaghafillulah. Jamaa: Si kuna mzee mmoja bwege nilitaka kumposa mwanae akanikatalia, mimi nikamuulia mbali.
Mzee: Karibu baba, unataka harusi lini? Mimi sina tabu, mke tu umepata! Mkeo huyu hapa baba! 

Jamaa mmoja aliyekuwa kichaa si alionekana kapona akaruhusiwa kutoka hospitali:

Madaktari wakamchukua katika gari la wagonjwa hadi mtaani kwake kisha wakasimamisha gari karibu na nyumbani kwake na kuulizwa, 
unapakumbuka kwako?” 
Akajibu “Ndio napakumbuka nyumba yangu ilee”, 
Wakatoka wanafunzi wawili katika ile nyumba wamevaa sare za shule, jamaa akasema,
Wanangu walee wanatoka wanaenda shule”, 
Mara akatoka mwanamke kabeba kikapu, jamaa akasema,
Na mke wangu yulee anatoka anaenda sokoni”, Ghafla akatoka mwanamume kavaa tai na kabeba brifkesi, jamaa akasema,
Enhee! na mimi yulee naenda kazini!

Mama kapanda daladala na mwanae wa miaka miwili, akataka kumnyonyesha, pembeni kakaa na njemba moja:

Mama: Nyonya basi mwanangu
Mtoto: (Anatingisha mabega kumaanisha hataki)
Mama: Au nimpe anko
Mtoto: (Analia) sitaki (anadaka nyonyo anaendelea). 

Punde akaacha tena kunyonya
Mama: Nitampa anko kama hautaki
Mama: Nimpe
Njemba: ahaaaa mama kuwa na msimamo basi nshapitiliza vituo vitatu kama unanipa nipe au kama vipi nishuke kituo kinachofuata
Mama: Heeeh?

UMESIKIA MAAJABU YA PANYA HAWA


Umesikia maajabu ya panya hawa?
Panya hao waliogunduliwa/fundishwa chini Tanzania katika chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine mkoani Morogoro wana uwezo wa ajabu.

Panya hao wana uwezo wa kugundua mabomu yaliyotegwa aridhini, pia panya hao wana uwezo wa kugundua vimelea vya ugonjwa wa kifua kikuu kupitia koozi la mgonjwa. 

JE WAJUA HILI :VUVUZELA NDANI YA KAMUSI YA OXFORD?

Kamusi maarufu ya kiingereza ya Oxford imeliingiza jina la Vuvuzela katika kamusi yake ya kiingereza na kuanza kutumika katika lugha hiyo. Vuvuzela ni kati ya maneno 2,000 mapya ambayo yameingizwa katika kamusi hiyo. Vuvuzela ni tarumbeta la plastiki na lilipata umaarufu sana duniani wakati wa fainali za soka za kombe la dunia zilizofanyika nchini Afrika Kusini mwaka huu.
LIKE PAGE YETU HAPA

HAPA NDIO KWA MWALIMU NYERERE

Hapa ndipo nyumbani kwa baba wa Taifa Hayati Mwalimu JK Nyerere, nyumba ya mwalimu ipo Butiama mkoa wa Mara na ndipo  alipozikiwa. Mwalimu Nyerere alikuwa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na alikuwa kiongozi wa mfano Afrika na Duniani kwa kuwa kiongozi muadilifu.
fahamu zaidi kwa kulike hapa

Je wajua kuhusiana na kipepeo?


Unajua kwamba miguu ya mdudu kipepeo ina uwezo wa kutambua aina ya chakula? Mdudu huyu mwenye uwezo wa kuluka, chakula chake kikuu ni maua. Miguu yake ina uwezo wa ajabu katika kutambua wa aina ya chakula. Mdudu huyo ana uwezo wa kutambua aina ya chakula kwa kutumia miguu yake miwili ya mbele. Kipepeo huwa ana miguu sita.

Monday 29 December 2014

Kichekesho cha Mlevi na Mchungaji Kanisani

Waumini waliambiwa watoe michango ili wazungushie ukuta eneo la makaburi.
Mchungaji akauliza kuna mtu ana swali?
Mlevi akauliza “Je kuna Marehemu yoyote aliyewahi kutoroka? Kama hakuna, ukuta wa nini sasa? Au ndio ufisadi hadi kwenye makaburi…?
Mchungaji kimyaaaaa!

Vichekesho kati ya mume na mke kanisani

Vichekesho kati ya mume na mke kanisani Je unajua vichekesho kanisani? ulishasikia mojawapo, hebu fuatilia hii hapa.
Kulikuwa na familia moja ya wacha Mungu vizuri tu pale Dar es salaam. Walikuwa wakisali kanisa moja la kilokole.  Mwanaume alikuwa na tabia ya kulala usingizi kila akiingia kanisani kusali. Siku moja mke wake akagundua dawa ya kumfanya jamaa aache kabisa tabia hiyo mbaya ya kulala kanisani. Unajua ni dawa gani hiyo?
Kukiwa tu ndo ibada imeanza, jamaa alianza kuuchapa usingizi na mke bila kukawia akamminya kwa haraka akamwambia,

Mtoto wa Miezi Tisa Ashitakiwa Kwa Jaribio la Mauaji Pakistani

Mtoto wa Miezi Tisa Ashitakiwa Kwa Jaribio la Mauaji Pakistani
Mtoto wa miezi tosa (9) mafichoni kule LAHORE Pakistan kwa sababu ana kesi ya kujibu. Mtoto huyo pichani ambaye hata hawezi kunyanyua chupa yake ya maziwa anadaiwa kushiriki kwenye jaribio la mauaji.
Baby huyo anayeitwa Musa Khan sasa yuko mafichoni kwani polisi wanamtafuta. Wiki iliyopita mtoto huyo alipelekwa mahakamani na kutajiwa kesi hiyo ya jaribio la mauaji katika mojawapo ya mahakama mjini LAHORE.
Pamoja na mtoto huyo Baba yake na Babu yake wanahukumiwa pia. Sakata hilo lilianza pale polisi mmoja na mfanyakazi wa kampuni moja ya gesi aliyekuwa anakusanya bili za muda mrefu waliporushiwa mawe na waandamanaji wanaopinga kupunguzwa kwa gesi na kupandishwa bei.
Kesi ya kichanga hiki inaonyesha wazi udhaifu ulioko kwenye sheria za PAkistani
Hata hivyo taarifa za hivi punde kutoka LAHORE, Pakistani zinasema kuwa mahakama hiyo imemfutia kesi mtoto huyo..
like page yetu kwa taarifa zaidi

Je wajua mwanamke mwenye ndevu nyingi kuliko wote duniani?

Je wajua mwanamke mwenye ndevu nyingi kuliko wote duniani? Annie Jones ambaye ni mzaliwa wa Virginia, Marekani ndie mwanamke mwenye ndevu nyingi kuliko wote duniani? Alizaliwa tarehe 14, 1865  akiwa amefunikwa na wingu la nywele mpaka wazazi wake wakamwita “ESAU”. Chanzo: http://f-r-e-a-k-s.tumblr.com/ Wanawake wengine wenye ndefu nyingi ni: Vivian
like page yetu kwa habari zaidi

Friday 12 December 2014

Lwakatare wa Chadema, Ludovick waibwaga Serikali mahakamani

Dar es Salaam.
Mahakama ya Rufani imetupilia mbali maombi ya marejeo kuhusu uhalali wa uamuzi wa Mahakama Kuu Dar es Salaam kuwafutia mashtaka ya ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare na mwenzake Joseph Ludovick Rwezahura.
Hatua hiyo ya mahakama imefanya kiongozi huyo wa Chadema na mwenzake kuibwaga Serikali kwa mara ya pili mahakamani katika mashitaka dhidi yao.
Maombi hayo namba 5 ya mwaka 2014, yalifunguliwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) katika Mahakama ya Rufani akipinga uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kufumfutia mashtaka ya ugaidi yaliyokuwa yakimkabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Uamuzi wa kutupilia mbali maombi hayo ulisomwa jana na Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufani, Zahra Maruma kwa niaba ya Jopo la Majaji watatu wa mahakama hiyo lililokuwa limepangwa kusikiliza maombi hayo.
Majaji hao ni Nathalia Kimaro (kiongozi wa jopo), William Mandia na Profesa Ibrahimu Juma.
Mahakama hiyo ilifikia uamuzi huo baada ya kujiridhisha kuwa maombi hayo yalikuwa na dosari za kisheria kutokana na DPP kutoambatanisha mwenendo wa uamuzi wa Mahakama Kuu aliokuwa akiupinga.
Dosari hiyo iliibuliwa na Jaji Prosefa Juma katika tarehe ambayo maombi hayo yalikuwa yamepangwa kusikilizwa ambapo alihoji iwapo ni halali kusikiliza maombi hayo bila kuwepo kwa mwenendo huo.
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Angaza Mwipopo akisaidiana na Wakili Serikali Mwandamizi, Hashim Ngole, alijibu kuwa wanachopinga ni uamuzi wa mahakama kufuta mashtaka katika kesi ambayo haikuwa mbele yake.
Wakili Angaza alidai kwamba kutokuwepo kwa mwenendo huo hakuathiri na kwamba mahakama ina uwezo wa kuyasikiliza maombi hayo hata bila kuwepo kwa mwenendo huo.
Akijibu hoja hizo, Wakili wa Lwakatare, Peter Kibatala alisema kuwa suala la mwenendo wa uamuzi unaopingwa ni miongoni mwa hoja za pingamizi lake la awali dhidi ya maombi hayo.
Wakili Kibatala alidai kuwa kutokuwepo kwa mwenendo huo ni dosari ambayo ina athari kubwa kiasi kwamba mahakama haitakuwa na uwezo wa kutoa kile kinachoombwa.
Alisisitiza kuwa kutokuwepo kwa kumbukumbu za mwenendo huo ni athari ambayo tiba yake ni mahakama kuyatupilia mbali maombi hayo.
Wakili Mwipopo alisisitiza kuwa kwa mujibu wa Kanuni ya 65 ya Kanuni za Mahakama ya Rufani, siyo lazima kuambatanisha mwenendo katika maombi na kwamba nyaraka za msingi kwa mujibu wa kanuni hiyo ni hati ya kiapo, ambavyo wameviambatanisha.
Hata hivyo, kupitia uamuzi wake jana, mahakama ilisema kuwa msimamo wa kisheria kwa mujibu wa kifungu cha 4 (3) cha Sheria ya Mamlaka ya Mahakama ya Rufani ni lazima kuambatanisha mwenendo wa uamuzi unaopingwa, uamuzi na amri ya mahakama katika maombi ya marejeo.
“Kutokana na kasoro hiyo ya kutokuwepo kwa mwenendo wa uamuzi unaopingwa, tunatupilia mbali maombi haya,” ilisema mahakama katika uamuzi wake.
Katika maombi hayo, DPP alikuwa akiiomba Mahakama ya Rufani iitishe majalada ya kesi hiyo na kuchunguza uhalali wa uamuzi wa Mahakama Kuu kuwafutia washtakiwa hao mashtaka ya ugaidi na kisha ifute uamuzi huo wa Mahakama Kuu na amri zote ilizozitoa. Pamoja na mambo mengine, DPP alikuwa akidai kuwa haikuwa sahihi Mahakama Kuu kuamua kuwa mashtaka hayo hayakuwa halali, kwani hapakuwa na taarifa zilizowasilishwa dhidi ya washtakiwa, ambazo Mahakama Kuu ingezizingatia katika kuamua uhalali wake.
Kulingana na uamuzi huo, DPP anaweza kufungua tena maombi hayo baada ya kurekebisha kasoro hiyo, lakini baada ya kuomba kibali cha mahakama kufungua marejeo hayo nje ya muda wa kawaida kisheria.
Akizungumzia kesi hiyo, Lwakatare alisema: “Kwanza namshukuru sana Mungu kwa kuniwezesha kushinda kesi hii…; kusema kweli ilikuwa kesi ngumu na mbaya, hasa ikizingatiwa kwamba ilikuwa ndiyo kesi ya kwanza ya ugaidi kufunguliwa hapa nchini.”
Lwakatare aliongeza: “Nawashukuru mawakili wangu ambao wamekuwa wakisimamia kesi hii pamoja na makahama pia kwa kutenda haki leo (jana). Kama ungefanyika uamuzi tofauti na huu, basi ningebaki Segerea. Pia, haki hiyo imeweza kutendeka kutokana na misingi ya kesi husika kuwa ya kusuasua. Kesi ilifunguliwa kwa jabza na shinikizo la kisiasa.”
Alieleza kuwa, licha ya shinikizo hilo, haki imeweza kutawala na ameshinda kesi hiyo mbali na misukusuko aliyopitia.
Alisema kwamba anatumaini makahama itaendelea kutoa hati katika kutoa uamuzi wa kesi yake iliyobaki katika Makahama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Naye Wakili Kibatala alisema kuwa kwa hali ilivyo suala hilo limekwisha na kwamba DPP hana mwanya wa kurudi tena na maombi hayo.
Alifafanua kuwa kwa kawaida maombi ya marejeo hufunguliwa katika muda wa siku 60 tangu siku ya kutolewa kwa uamuzi unaopingwa na kwamba, nje ya muda huo mwombaji analazimika kuomba kibali cha Mahakama kufungua maombi nje ya muda na kutoa sababu za kuridhisha.
“Siku 60 tayari zimeshakwisha, hivyo DPP akitaka kurudi tena ni lazima aombe kibali na atoe sababu za kuiridhisha Mahakama. Sababu za kuridhisha ni pamoja na ugonjwa, au kuchelewa kupata nakala ya uamuzi na mwenendo kutoka mahakamani, lakini siyo kwa uzembe,” alisema.
Lwakatare na Ludovick walikuwa wakikabiliwa na mashtaka manne, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, matatu kati yake yakiwa ya ugaidi na moja la kawaida la jinai.
Mashtaka hayo ya ugaidi yalikuwa ni kupanga kumteka aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky na kisha kumdhuru kwa sumu, kushiriki mkutano wa vitendo vya ugaidi (kwa washtakiwa wote) na kuhamasisha vitendo vya ugaidi lililokuwa likimkabili Lwakatare pekee.
Shtaka lingine la jinai lilikuwa ni kula njama ya kutenda makosa, ambalo lilikuwa likiwakabili wote kwa pamoja na bado linaendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Hata hivyo, Mei 8, mwaka huu Jaji Lawrence Kaduri wa Mahakama Kuu aliwafutia mashtaka ya ugaidi, baada ya mawakili wa Lwakatare kufungua maombi wakipinga uamuzi wa DPP kuwafutia mashtaka katika kesi ya awali na kisha kuwakamata na kuwafungulia mashtaka hayohayo.

Chadema kupinga uchaguzi wa mitaa leo

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) mkoa wa Kilimanjaro, kimepitisha azimio la kwenda mahakamani kusimamisha uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Desemba 14 mwaka huu, hadi hapo Tamisemi itakapotoa haki ya kurejeshwa kwa wapiga kura 517 na wagombea wake 52 walioenguliwa.

Friday 5 December 2014

Je wajua baba mdogo kuliko wote duniani?

Je wajua baba mdogo kuliko wote duniani? Baba mdogo kuliko wote duniani huyu hapa na mke wake

Je wajua Baba mzee mkongwe kuliko wote duniani ?

Baba mzee mkongwe kuliko wote duniani

Je Wajua Nchi 5 Hatari kwa Wanawake Kuishi Duniani?

Nchi Hatari Kwa Wanawake Kuishi DunianiLONDON (TrustLaw) imebaini katika tafiti zao kuwa Afghanistan, Kongo na Pakistan ni nchi hatari zaidi kwa wanawake kuishi duniani kutokana na mlipuko wa vitisho kuanzia unyanyasaji, ubakaji, afya duni, Nk. Kura ya maoni iliyofanywa na mtaalam wa Thomson Reuters Foundation
India na Somalia katika nafasi ya nne na ya tano, kwa mtiririko huo,
TrustLaw iliuliza wataalam wa jinsia 213 kutoka mabara matano juu ya mtazamo wa jumla wa hatari kama vile: afya duni, unyanyasaji wa kijinsia, mahusiano yasiyo ya kingono, kitamaduni au kidini, ukosefu  wa rasilimali na biashara ya binadamu.
Nchi Tano Hatari Duniani kwa wanawake ni:
1. Afghanistan
2. CONGO
3. PAKISTAN
4. INDIA
5. SOMALIA
like hapa kwa habari zaidi

Je, wajua kwamba kuna mambo haya yanayokuzunguka?

1. Je, wajua kwamba binadamu pamoja na akili zake zote, pamoja na mbwembwe zake nyingi, bado hana uwezo wa kufikisha ulimi kwenye kiwiko cha mkono wake?
2. Je, wajua kwamba kama piza zinazoliwa kwenye bara la Amerika kwa siku zingepangwa zingeweza kuchukua eneo lenye ukubwa wa hekta 18?
3. Je, wajua kwamba kila binadamu ana alama tofauti kabisa na za kipekee katika ulimi wake (tongue-prints) kama zilivyo za vidole?
4. Je, wajua kuwa mnyama aina ya mamba huwa hana uwezo wa kutoa ulimi wake nje kutokana na maumbile yake?
5. Je, wajua kuwa farasi na panya ndio wanyama pekee wasiotapika?
6. Je, wajua kuwa jicho la mbuni ni kubwa kuliko ubongo wake?
 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets