Pages

Friday 3 April 2015

Wataalamu wagundua sayari inayofanana na yetu, hatuwezi kufika

MOJA kati ya sayari nane mpya zilizo nje ya mfumo wa jua (letu) imeonekana kuwa na mazingira kama dunia yetu.
Sayari hizo ambazo ziko umbali wa miaka ya mianga 475 zimeonwa na darubini maalumu ya kuangalia mifumo ya nyota mbali na nyota yetu, inayomilikiwa na Wamarekani ya Kepler.
Kwa Mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Anga za Juu la Marekani (NASA)  imesema sayari tatu zinafanana na dunia yetu kutokana na hesabu za umbali kutoka katika jua (lao) lakini moja ndio inaonekana kuwa na  mazingira yanayofanana na dunia na ina joto la juu kidogo.
Taarifa hiyo ya wataalamu wanaoangalia taarifa kuhusu sayari nyingine nje ya mfumo wa sayari yetu zimetolewa katika mkutano wa wanajimu wa Marekani(American Astronomical Society)
Sayari hizo 3 ambazo zimeingia katika jedwali la Kepler zinafanya sayari zinazoonekana kufaa kama dunia yetu kuwa nane.
Wataalamu wamesema kwamba  moja ya sayari inayotambulika kama Kepler 438b,yumkini ni karibu sawa na dunia yetu tunayoishi kuliko sayari nyingine ya Kepler 186f .
Ikiwa ni kubwa kwa asilimia takaribani  12, sayari hiyo mpya ni kubwa kuliko 186f lakini iko karibu sana na joto la dunia yetu ikipata asilimia 40 ya joto kutoka katika jua lake  kuliko sisi.
Maana yake ni kuwa kama tutasimama katika uso wa sayari 438b tutajisikia joto zaidi kuliko hapa duniani, kwa mujibu wa Dk Doug Caldwell kutoka taasisi ya  Seti (Search for Extra-Terrestrial Intelligence) ya California.
"Na kwa kuwa karibu na nyota yake anga lake litaonekana jekundu  kuliko la kwetu," anasema Dk Caldwell .
Kuonekana kwa sayari hizo nyingine kunafanya idadi  kamili ya sayari zinazoweza kuwa na uhai kama yetu kuwa nane.
Pamoja na sayari hizo kuonekana ni ngumu sana kwa mwanadamu kufika huko kutokana na ukweli kuwa zipo umbali wa miaka ya miaka 475 na kwamba haijajulikana ni aina gani ya madini zimetengeneza sayari hizo.
Picha zilizoletwa na darubini ya Kepler ambayo iko nyuma ya dunia ikichungulia ndani ya anga wakati, dunia inazunguka jua, inatumika kutambua sayari hizo kwa kutumia mfumo wa kuangalia kile kinachoitwa kisayansi "transits".
Hii inamaananisha kuona mwanga nyota unaominywa wakati sayari inapita mbele yake.
Darubini ya kepler iliyotupwa hewani mwaka 2009 kwa lengo la kuytafuta sayari zinazofanana na dunia yetu mwaka jana pekee ilileta taarifa za uwapo wa sayari ambazo kitaalamu wanaziita, exoplanets, 715
Ili kuthibitisha kwamba hizo ni sayari zinazofanana na yetu au la wataalamu hutumia takwimu za ziada kutoka katika darubini zinazoangalia dunia kwa lengo la kuzijua vyema sayari hizo.
Miongoni mwa mambo wanayofanya ni kuona sayari hizo zina ukubwa gani na ziko mbali kutoka katika jua la mzingo wao kwa kiasi gani.
Imeelezwa si kila kitu kinachozunguka nyota huwa ni sayari.
Takwimu zaidi zinaonesha kwamba wataalamu wa NASA na wenzao wanakazi kubwa ya kuabngalia maumbo mengin zaidi ya 500 yaliyoletewa taarifa na Kepler.
Mtaalamu wa mambo ya anga za juu Fergal Mullally amesema uchunguzi na utafiti ukiendeleza zaidi huenda sayari hizo zikaonekana kwambna hazifanani na dunia.
Aidha alisema kuna kuweza kuwa na mabadiliko kwa namna zinavyojiingiza kwa ndani au nje ya uwezekano wa kuwa na maisha.
Ili kutambua kama sayari zinafaa kuishi ni lazima wanasayansi waangalie umbali wa sayari hiyo kutoka katika jua lake, umbali utakaowezesha kuwa na maji na wala si umbali unaofanya maji hayo kuganda
Kazi ya kutambua uhai katika sayari hiyo inafanyika kwa kuhisi zaidi kw akuchambua nyaraka mbalimbali na sheria za kifizikia na kemikali
Kwa mujibu wa Dk Cardwell,  ni sayari tatu tu mpya kati ya nane zinahisia hizo  na ni moja tu kati ya mbili inaonekana kuwa na wajihi wa dunia tunayoishi sisi.
Hata hivyo amesema kwamba taarifa za ndani zaidi ni ngumu kupatikana.
"Kutoka katika darubini ya Kepler ,vipimo vyake na vipimo vingine tunavyovitumia hatujui kama sayari hizi zina bahari na samaki na bara lenye miti," alisema Dk Caldwell wakati akizungumza na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC).
"Tunachojua sasa ni nishati inayopoipkelewa kutoka katika nyota yao(jua).
"Kwa hiyo tunaweza kusema: Vyema, zina ukubwa wa sayari yetu inaonekana ina miamba na nishati wanayopata ni sawa na ya kwetu.
"Wakati tukijaza mapengo haya ya taarifa, tunajifunza nini maana ya kuwa na dunia kama yetu kwa namna nyingine."
Akizungumza katika tukio jingine, Profesa Debra Fischer kutoka chuo kikuu cha Yale alisema anakumbuka mara ya kwanza wanaona sayari hizo na mazungumzo ya wataalamu miongo miwili iliyopita.
"Nakumbuka wanajimu waliokuwa na shaka sana kuhusu hilo," alisema.
"Tulijikuta tukisema labda picha hiyo  ni sawa na Star Trek.Nilijisikia vibaya sana."
Prof Fischer amesema kwamba darubini hiyo Kepler imeleta taarifa nyingi zenye heshima kubwa.
"Tunazungumzia sayari nje ya sayari yetu na mfumo wetu  na tunaweza hilo kwa kutumia darubini yenye nguvu kubwa.
"Na tunaweza kuchora grafu na kutoa taswira na kufanya majadiliano ya kisayansi. Hili ni tukio la kushangaza sana.

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets