Pages

Wednesday 17 June 2015

MWANAANGA WA KWANZA AFRIKA KWENDA MWEZINI ATOA SEMINA KWA WANAFUNZI WA SEKONDARI DAR.


 Meneja Mahusiano wa Multichoice Tanzania Barbara Kambogi akizungumza na wanafunzi wa shule mbalimbali za Sekondari za jijini Dar  kuhusiana na shindano kubwa lililoshirikisha wanafunzi kutoka nchi zote za Afrika la kuandika Insha na kuchora picha kuhusiana na mambo ya Anga linaloitwa DStv EUTELSAT STAR AWARDS ambapo mshindi wake atapata nafasi ya kwenda Paris nchini Ufaransa na wazazi wake kushuhudia namna safari ya kwenda mwezini inavyofanyika kabla ya kumkaribisha Mwanaanga wa Kwanza Afrika Kwenda mwezini Patrick Baudry ambaye atazungumza nao kuhusiana na uzoefu wake kuhusiana na masuala ya Anga.
Barbara amesema kwamba mshindi wa shindano hilolililodhaminiwa na Dstv atatangazwa  hapo kesho katika hafla maalum ya chakula cha jioni itakayofanyika katika Hotel ya Hyatt Regency Kilimanjaro.

Mwanaanga wa kwanza kutoka Barani Afrika kwenda mwezini Patrick Baudry leo ametoa mafunzo kwa wanafunzi shule za Sekondari za jijini Dar es Salaam juu ya mpangilio mzima wa safari ya kwenda mwezini na kurudi tena duniani.
Baudry ametoa mafunzo hayo katika ukumbi wa Nkurumah ikiwa ni semina maalum kwa wanafunzi wa shule za sekondari hapa nchini ambao wameshiriki kwenye shindano kubwa la kuandika Insha na kuchora picha kuhusiana na masuala ya Anga. Baudry mwenye umri wa miaka 66 ni mzaliwa wa Cameroon.
Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Hindu Mandal.
 Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Sekondari Jangwani wakitega sikio kwa umakini.
Baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wakimsikiliza kwa makini Mwanaanga Patrick Baudry (hayupo pichani) aliyezungumza na wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Ukumbi wa Nkuruma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam leo.
 Patrick  Baudry akijibu maswali aliyokuwa akiulizwa na wanafunzi hao. Kulia ni Barbara Kambogi.
 Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Jangwani akiuliza Swali kwa Mwanaanga Patrick Baudry (hayupo pichani) wakati akizungumza na Wanafunzi jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya Walimu wa shule mbalimbali nchini waliombatana na wanafunzi wao.
 Patrick Baudry akitia saini Autograph za Wanafunzi hao baada ya kumaliza kipindi cha maswali na majibu.

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets