Pages

Friday 28 August 2015

Je Wajua Mnyama Mwenye Mdomo Mkubwa Kuliko Wote Duniani?

Mnyama Mwenye Mdomo Mkubwa Kuliko Wote Duniani ni Kiboko.
Kiboko ndiye mpaka sasa hivi anayeongoza duniani kwa kuwa na mdomo mkubwa. Pia anaongoza kwa kupanua mdomo anapopiga miayo. Mdomo wake unaweza kupanuka mpaka digrii 170 ambayo ni sawa na mstari ulionyooka ukipungua kwa digrii kumi (10) tu.

Mnyama huyu anapatikana sehemu Ngorongoro, Ruaha, na sehemu zingine za Afrika. Kiboko anaishi majini na Nchi kavu. Muda mwingi majini na nyakati za jioni anatoka kwenda kutafuta malisho. Kiboko muda mwingi anapenda kukaa kipweke na kiboko wa kiume ni mzito kuliko wa kike. Kiboko anaweza kufikia tani 3 na kumfanya kuwa mnyama wa nchi kavu wa tatu kwa uzito duniani baada ya Tembo na Kifaru. Kiboko pia ni mnyama wa nchi kavu wa pili duniani kwa ukubwa baada ya Tembo. Kiboko anakula tu majani na hivyo kuwa sawa na Ngombe, Mbuzi, Nyati, Swala, Pundamilia, na jamii yote ya wanyama wannaokula majani tu.
like page kwa habari zaidi

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets