Pages

Sunday 10 August 2014

Kuna jamaa mmoja alikuwa kila siku usiku akilala anaota NGEDERE na PANYA wanacheza mpira ikabidi siku moja aende hospital kumuona dokta alipofika hospital mazungumzo yakawa hivi:-
JAMAA: "Dokta mimi nimekuja ninasumbuliwa na ndoto kila siku usiku nikilala naota Ngedere na Panya wanacheza mpira utanisaidiaje?"
DOKTA: "Kwa hilo tatizo lako ulilosema inabidi nikupe hizi dawa ukifika nyumbani uzimeze, ukizimeza kuanzia leo hauto ota tena ndoto hizo sawa!"
JAMAA: "Sawa dokta ila itabidi nianze kuzimeza kesho kwakuwa leo ndio Fainali nataka nijue nani atashinda katika mechi ya leo"
- Dokta alibaki anashangaa!


Dir Kuna mgonjwa mmoja alikwenda hospitali kupimwa alipopimwa na dokta akagundulika anaumwa ugonjwa wa kiharusi mambo yakawa hivi:-
DOKTA: "Nimekupima nimekukuta unaumwa Kiharusi"
MGONJWA: "Ni kweli dokta ndio mana nilikuwa nina hamu sana ya kutaka kuoa! Kumbe naumwa kiharusi"
- Dokta alibaki anashangaa!
Dir - Kuna Teja mmoja alikuwa amelala chini katika kituo cha Mabasi wananchi kibao wakamzunguka kumuangalia na kila mmoja akaanza kujiuliza kwanini kalala pale chini? Kila mwananchi akaanza kutoa maoni yake:-
MWANANCHI 1: "Jamani huyu atakuwa anaumwa, tumpelekeni kwanza hospital"
MWANANCHI 2: "Mimi ninachoona tumpelekeni kwanza Polisi"
Ghafla ikasikika sauti ya Bibi mmoja akisema:-
BIBI: "Sikilizeni jamani Pengine ananjaa huyu hajala hebu mtu mmoja aende akamnunulie chips na soda ale"
Baada ya yule Bibi kusema vile mara yule mteja akainua kichwa na kusema:-
TEJA: "Jamani msikilizeni Bibi anavyosema"
Wananchi wote waliokuwa wamemzunguka wakaangusha kicheko mmoja wao akasikika akisema "KUMBE JAMAA ALIKUWA ANANJAA KISHAVUTA MI UNGA YAKE SASA UBAO UNAMCHARAZA" hahahaaaa!
Dir kuna wanandoa wawili walikuwa wanaish nyumba moja lakini walikuwa wanaugomvi wakawa hawaelewani ndan ya nyumba yao mpaka wakafikia hatua ya kuwekeana mipaka chumbani ikawa kati yao kama kuna mmoja anashida na mwenzake anamuandikia mwenzie ktk karatasi walikuwa hawaongei. Sasa siku moja usiku mwanaume alikuwa anasafar kesho yake asubuh mapema akamwambia mke wake amuamshe asubuh mapema saa12, wakalala ilipofika asubuh sa12 yule mwanamke akaamka akachukua karatasi akamuandikia "mume wangu amka sa12 imeshafika" halaf akarud kulala yule mwanaume akaamka baadae akamwambia "Mke wangu mbona hukuniamsha?" mwanamke akasema huoni nimekuandikia ktk hilo karatasi. BASI TOKEA HAPO WAKAANZA KUONGEA

Dir - kuna hospital moja ya vichaa ilikuwa imeishiwa dawa za kuwapima vichaa akili zao kama wamepona, ikabidi doctor achore alama ya mlango ukutani halaf akawaambia wale vichaa "ATAKAE WEZA KUPITA HAPA AKAONDOKA HUYO ATAKUWA AMEPONA ANARUHUSIWA KWENDA NYUMBANI" basi wale vchaa wote walivyosikia vile wakaanza kugombania kupita ktk ule mchoro, kuna kichaa m1 yeye hakwenda kugombania akabaki anawatizama pemben huku anawacheka wenzie yule Dokta akajua pengine huyu kishapona akamuuliza "WE UNACHEKA NINI?" akamjibu dokta "NAWASHANGAA HAO WANAGOMBANIA KUTOKA NJE WAKATI FUNGUO NINAYO MIMI".
 
 
 

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets