Pages

Saturday 25 October 2014

Haya ndiyo majengo saba marefu zaidi duniani, si mchezo

Tunakuorodhoshea majengo saba marefu kuliko yote duniani. Dubai ndiyo inabeba sifa ya kuwa na jengo lililopanda angani kuliko yote hapa duniani.

7.Petronas Tower: Kuala Lumpur, Malaysia
Majengo ya  Petronas Twin Towers
Pia hujulikana kama Petronas Twin Towers, minara pacha hii ndiyo majengo pacha marefu zaidi duniani, yana urefu wa
futi 1,483na ghorofa 88. Ujenzi wake kunako miaka ya 90, uliashiria ukuaji mkubwa wa uchumi wa Malaysia na kuliingiza taifa hilo miongoni mwa mataifa yanayoibukia kiuchumi duniani.














6.International Commerce Centre: Hong Kong, China
  International Commerce Centre: Hong Kong, China
International Commerce Centre lina urefu wa futi 1,588, na jumla ya ghorofa 118. Ndilo jengo refu zaidi Hong Kong.












5.Shanghai World Financial Center: Shanghai, China
Shanghai World Financial Centre
Shanghai World Financial Centre lina nafasi za ofisi, mahoteli na paa maalum lenye sehemu ya kuangalia mandhari na maduka kwenye ghorofa ya kwanza. Lina urefu wa futi 1,614 na ghorofa 101. Pia lina paa maalum la kuangalia mandhari lililoko juu zaidi duniani, futi 1,555 kutoka ardhini.













4.Taipei 101: Taipei, Taiwan
Tapei 101
Jengo la Tapei 101 linanyanyuka futi 1,669. Lina ghorofa tano za chini y ardhi na 101 kwenda angani. Ndilo jengo refu zaidi duniani lililojengwa kwa kuzingatia ubora wa mazingira.Wakati wa sherehe za kitaifa, fashi fashi huwashwa kwenye jengo hili.













3.One World Trade Center: New York, NY
One World Center
Pia hujulikana kama Freedom Tower, jengo hili lina urefu wa futi 1,776 feet, na lina ghorofa 104, na kulifanya kuwa refu zaidi katika mataifa ya magharibi. Lilijengwa kufikia futi 1776 kama kumbu kumbu ya mwaka ambao Marekani ilipata uhuru wake.






2.Makkah Royal Clock Tower Hotel: Mecca, Saudi Arabia
Makkah Royal Clock Tower Hotel: Mecca, Saudi Arabia
Jengo linaitwa The Makkah Royal Clock Tower Hotel, lilijengwa katika jitihada za kuubadilisha mji mtukufu wa Makkah kuwa wa kisasa zaidi. Lina sifa kadhaa – ndiyo hoteli ndefu zaidi duniani, mnara wa saa ulioko juu zaidi duniani, na pia saa kubwa zaidi duniani. Lina urefu wa futi 1,972 na ghorofa 120.

1.Burj Khalifa: Dubai, United Arab Emirates
Burj Khalifa: Dubai, United Arab Emirates
Jina lake ni Burj Khalifa, awali likijulikana kama Burj Dubai, hili ndilo baba na mama wa majengo kwa urefu duniani. Lina urefu wa futi 2,723 na ghorofa 163. Kazi ya ujenzi ilichukua miaka mitano, na ilikamilika mwaka 2009 katikati ya Dubai.

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets