Pages

Saturday 25 October 2014

WILAYA ya Rungwe Jijini Mbeya ina mambo mengi ya kustaajabisha na miongoni mwa mambo hayo yapo kwenye Mto Kiwira. Mto Kiwira unazidi kupanda chati kuliko mito mingine wilayani humo kutokana na kuwapo kwa Daraja la Mungu. Lakini pia karibu na daraja hilo yapo maajabu mengine yakiwamo ya chekeche la uchafu unaokusanywa na maji kabla ya kuingia eneo maarufu la Kijungu. Kijungu nayo ni sehemu ya Mto Kiwira, ni eneo la ajabu kwa sababu mwamba wake umeumba kitu kama chungu kinachopokea maji yote na kuyapeleka chini bila kupitisha juu ya mwamba. Inaelezwa kwamba mtu anayetaka kuvuka salama kwenye mwamba juu ya Kijungu kutoka upande wa Mashariki lazima atumie mguu mmoja wa kulia na akitokea Magharibi atumie mguu wa kushoto tu ili asitumbukie. Maajabu mengine ni kuwapo kwa taarifa zinazodai mtu akizama kwenye mto huo, lazima afuatwe mzamiaji mmoja aliyerithi kazi hiyo kutoka kwa aliyekuwa kiongozi wa kimila na kwamba bila huyo, aliyezama hawezi kuonekana mpaka siku saba zitakapopita. Lakini jambo kubwa linaloonekana na kustaajabisha ni kuwapo kwa daraja linaloaminiwa na wakazi wa eneo hilo na wilaya nzima ya Rungwe kwamba lilitengenezwa na Mungu kwenye eneo la Mto Kiwira unapotenganisha Vijiji vya Lugombo kwa upande wa Mashariki mwa mto huo na kile cha Mboyo kilichopo Magharibi.

WILAYA ya Rungwe Jijini Mbeya ina mambo mengi ya kustaajabisha na miongoni mwa mambo hayo yapo kwenye Mto Kiwira.
 Mto Kiwira unazidi kupanda chati kuliko mito mingine wilayani humo kutokana na kuwapo kwa Daraja la Mungu.
 Lakini pia karibu na daraja hilo yapo maajabu mengine yakiwamo ya chekeche la uchafu unaokusanywa na maji  kabla ya kuingia eneo maarufu la Kijungu.
 Kijungu nayo ni sehemu ya Mto Kiwira, ni eneo la ajabu kwa sababu mwamba wake umeumba kitu kama chungu kinachopokea maji yote na kuyapeleka chini bila kupitisha juu ya mwamba.
Inaelezwa kwamba mtu anayetaka kuvuka salama kwenye mwamba juu ya Kijungu kutoka upande wa Mashariki lazima atumie mguu mmoja wa kulia na akitokea Magharibi atumie mguu wa kushoto tu ili asitumbukie.
Maajabu mengine ni kuwapo kwa taarifa zinazodai mtu akizama kwenye mto huo, lazima afuatwe mzamiaji mmoja aliyerithi kazi hiyo kutoka kwa aliyekuwa kiongozi wa kimila na kwamba bila huyo,  aliyezama hawezi kuonekana mpaka siku saba zitakapopita.
Lakini jambo kubwa linaloonekana na kustaajabisha ni  kuwapo kwa daraja  linaloaminiwa na wakazi wa eneo hilo na wilaya nzima ya Rungwe kwamba lilitengenezwa na Mungu  kwenye eneo la  Mto Kiwira unapotenganisha Vijiji vya Lugombo kwa upande wa Mashariki mwa mto huo na kile cha Mboyo  kilichopo Magharibi.
like page yetu kwa habari zaidi 

No comments:

Post a Comment

 

Blogger news

Blogroll

LIKE PAGE YETU KWA HABARI ZA KILA WAKATI

Receive all updates via Facebook. Just Click the Like Button Below

Powered By Blogger Widgets